IMANI



 Imani ni mtu kuamini Mungu. Neema ni Mungu kuamini mtu
Maisha ni kushirikiana, barabara mbili, hali ya kupeana na kuchukua ambayo inafanya uhusiano ulio na mazao bora. Bila ushirikiano huu vile tunajua, maisha hayawezi kuendelea. Hata Mungu, ingawa ni Mkuu na hagharimii yeyote, amechagua kukamilisha mapenzi yake kwa kushirikiana na binadamu. Nguvu na afya ya uhusiano wowote unategemea kila mmoja akitenda sehemu yake kwa njia isiyo ya uchoyo
.
Uhusiano ulio nao na Mungu, kinyume na imani zingine, sio kwa ajili yako. Imani ni kile unachompa Mungu ukitumai kitabalisha dunia yako. Neema, hata hivyo, ni kile Mungu anakupa, akitumai kitabadilsha dunia yake. Mungu ndiye tumaini lako … wewe ni wake. Kwa hivyo, weka imani yako na uamini Mungu wakati ambapo yeye pia ataweka imani yake kwako. Tumia neema zako za maisha ulizopewa na Mungu kufaidisha Ufalme wa Mungu na sio wako tu.
Ombi la Leo
Mungu, nisaidie kugundua kwamba uhusiano wetu ni njia mbili na kwamba sote tunategemeana kwa msaada tunaohitaji. Najua ninaweza kuweka imani yangu kwako kwa siku zangu za usoni na naomba uniamini na mipango yako. Kwa neema yako, sitakuangusha.
Maandiko ya Leo
Wakolosai 1:27 Mpango wa Mungu ni kuwajulisha watu wake siri hii kuu na tukufu ambayo ni kwa ajili ya watu wote. Na, siri yenyewe ndiyo hii: Kristo yuko ndani yenu, na jambo hilo lamaanisha kwamba ninyi mtaushiriki utukufu wa Mungu.
Waefeso 2:8 Maana, kwa neema ya Mungu mmekombolewa kwa njia ya imani. Jambo hili si matokeo ya juhudi zenu, bali ni zawadi ya Mungu.
Warumi 5:2 Kwa imani yetu, yeye ametuleta katika hali hii ya neema ya Mungu ambamo sasa tunaishi. Basi, tunajivunia tumaini tulilo nalo la kushiriki utukufu wa Mungu.
Maswali yanaweza kubadilika kutoka ujira mmoja wa maisha hadi mwingine; hata hivyo, majibu kila mara ni yale yale
Tunapokua tukupitia maisha, mara kwa mara tunabadilika katika ujira mmoja hadi mwingine. Kutoka shule ya watoto hadi shule ya msingi, kutoka shule ya upili hadi masomo ya juu, kutoka kukuza watoto hadi kustaafu, majira ya maisha huja na kuenda. Kwa kila sehemu ya maisha kunaweza kuwa na maswali mengi tunayokumbana nayo, mambo ambayo hatujawahi kabiliana nayo hapo awali.
Ingawa maswali hayo yanaweza kubalika kutoka ujira mmoja wa maisha hadi mwingine, majibu hubaki yaleyale. Neno hilo hilo la Mungu, mapenzi ya Mungu, na njia ya Mungu itakuwa mwongozo wako maishani. Heshima, tabia, unyenyekevu, uvumilivu, upendo, msamaha, kujizuilia, na imani itakuwa nguzo yako na udhibitisho wa uvumilivu katika maisha yako yote. Shiklilia majibu yale mepesi yatokayo katika Neno la Mungu.
Ombi la Leo
Bwana, ninaahidi kuweka Neno Lako karibu na mimi na kulificha ndani ya moy wangu ili nisitoke katika mapenzi Yako. Nitalifanya la kutafakari kila wakati na furaha yangu. Niongoze kupitia majira ya maisha na unipe amani yako kuchao.
Maandiko ya Leo
Waebrania 13:8 Yesu Kristo ni yuleyule, jana, leo na milele.
Wagalatia 5:22 Lakini matokeo ya kuongozwa na Roho ni mapendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu, …
Kuna uwezo kaitka chombo kilicho tupu
2 Wafalme 4 inatuambia hadithi ya mwanamke aliyekuwa na haja kuu. Akamjia nabii Elisha na akaamuriwa kumba vyombo vitupu kutoka kwa majirani wake. Elisha akamwambia ya kwamba Mungu atapaka kiwango kidogo cha mafuta aliyokuwa nayo na kujumulisha kujaza kila chombo kilichokuwa tupu. Kwanini vyombo vitupu? Vyombo vilivyojaa huenda vikawa vishafika siku zao kuu, kulingana na ni nini vimejazwa. Vyombo vilivyojaa nusu angalau vinaweza toa mchanganyiko wa Mungu na mwanadamu vikielekeza kumwagika chini kwa upako.hata hivyo, vyombo vitupu vinatoa fursa kuu ya kujazwa kabisa na upako wa kimiujiza wa Mungu. Maisha yetu ni chombo,tunakiinua kwa Mungu. Wakati mwingi tumejaa nusu ama tumejazwa kabisa na mambo mengine ambayo sio kuchagua kwa Mungu,ambayo huleta kung’ang’ana ama kushindana na upako ambao Mungu angelitaka kutumwagia ndani yetu. Je, ungependa kuondolewa mambo haya kidunia ili ujazwe na Mungu? Jimwage mwenyewe katika maombi na uruhusu upako mpya wa Roho Mtakatifu ujaze maisha yako.
Ombi la Leo
Baba, najitoa mwenyewe katika mambo haya ya ulimwengu na nikuuliza ujaze maisha yangu. Sitakata tamaa ninapojikuta niko tupu nikihitaji upako wako.
Maandiko ya Leo
2 Wafalme 4:1-7 Basi, mwanamke mmoja mingoni mwa wake za wana wa manabii alimlilia Elisha, akasema, Mtumishi wako mume wangu amekufa; nawe unajua ya kuwa mtumishi wako alikuwa mcha Bwana; na aliyemwia amekuja iliajitwalie wana wangu wawili kuwa watumwa. Elisha akamwambia, nikufanyie nini? Niambie; una kitu gani nyumbani? Akasema, mimi mjakazi wako sina kitu nyumbani, ila chupa ya mafuta. Akasema, nenda, ukatake vyombo huko nje kwa jirani zako wote, vyombo vitupu; wal usitake vichache. Kasha uingie ndani, ukajifungie mlango wewe na wanao, ukavimiminie mafuta vyombo vile vyote; navyo vilivyojaa ukavitenge. Basi akamwacha, akajifungia mlango yeye na wanawe; hao wakamletea vile vyombo, na yeye akamimina. Ikawa, vilipokwisha kujaa vile vyombo, akamwmbia mwanawe, niletee tena chombo. Akamwambia hakuna tena chombo. Mafuta yakakoma. Ndipo akaja akamwambia yule mtu wa Mungu. Naye akasema, nenda ukayauze mafuta haya, uilipe deni yako; nayo yaliyosalia uyatumie wewe na watoto wako.
Maisha ni fursa
Hebu wazia kuamka asubuhi moja bila kazi, gari, ama pengine nyumba. Hii yaweza kuonekana kama moja wapo ya siku za huzuni maishani mwako ama yaweza kuonekana kama moja wapo ya fursa kuu ya maisha. Hebu litafakari…ingawaje waweza kukosa ulichokuwa nacho na pengine haungechagua kukipoteza, hata hivyo, sasa uko na fursa ya kukibadilisha na kile unachotamani. Pengine, waweza kuijenga vyema zaidi wakati huu, ifanye tofauti kwa njia nyingine, na uishie kuwa na kitu kinachoambatana na mahitaji yako ya sasa ama siku za usoni. Hauwezi kila mara kuchagua kile unachopoteza lakini waweza chagua kufanya bidii kuelekea kubalisha hasara na kile bora zaidi.
Ombi la Leo
Ewe Bwana, nipe neema ya kuendeleza hasara zangu, na kuwacha majuto yangu mikononi Mwako na nibadilishe imani yangu Kwako. Nipe hekima ya kutazama kila siku kama fursa ya kufikia ukuu kwa ubora Wako.
Maandiko ya Leo
Wafilipi 3:13, 14 Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya dhawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.
Isaya 43:18-19 Msiyakumbuke mambo ya kwanza, wala msiyatafakari mambo ya zamani. Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.
Kwa pumzi yako ya mwisho waweza sema kwa ujasiri kwamba siku yako kuu bado iko mbele
Bila kutilia maanani ni nini tofauti za binadamu: mila, uzalendo, sehemu ya mtu maishani, kama mtu ni tajiri au masikini, kama mtu amesoma ama ni mpumbavu kabisa, ama hali za kuzaliwa kwetu, tuko na agano ambalo tutatimiza: agano na kifo.
Agano hili na kifo ndiyo sababu ni lazima tuhubirie ulimwengu, tukishiriki upendo wa Kristo na tuwakilishe uchaguzi wa kukubali ama kukataa upendo wa Mungu. Kwa wale wamkataao Kristo, kifo kitawashikilia hukumu ya kifo, lakini kwa Mkristo, kifo ndiyo njia ya amani ya milele, furaha, tumaini, na upendo. Tumaini lililo bora zaidi kwa Mkristo upande huu wa mbingu ni uhakikisho ya kwamba hata nini kitendeke maishani haya, bora zaidi bado yaja. Ni ya muhimu tuweke mtazamo wa umilele tunapotazamia maisha kama tunavyoyajua sasa kwa sababu kwa kweli siku yetu kuu bado iko mbele!
Ombi la Leo
Baba, ninashukuru sana kujua kwamba Unaniandalia makao. Kwa wakati wa ajabu nitakuona uso kwa uso na nijazwe na kuelewa kwa upendo wako na utukufu wa uwepo Wako. Ninapotazia maisha, nisaidie kuweka mtazamo wa umilele - kwa vile wakati yote yamesemwa na kutendwa, siku yangu kuu bado iko mbele.
Maandiko ya Leo
1 Wathesalonike 4:13-14 Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini. Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
Yohana 14:1-3 Yesu aliwaambia, "Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwaminini Mungu, niaminini na mimi pia. Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; la sivyo ningalikwisha waambieni. Sasa nakwenda kuwatayarishieni nafasi. Na nikienda na kuwatayarishieni nafasi, nitarudi na kuwachukueni kwangu, ili nanyi muwe pale nilipo mimi.
Luka Mtakatifu 21:28 Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia."
Kuza subira kuu ya kurudia
Waweza kuwa tayari umesikia kwamba ufanisi ni zaidi ya hatua moja na kwamba ufanisi mara kwa mara ni ya kwa wale ambao wanaweza kuvumilia hiyo hatua.
Maisha yamejawa na majaribu na makosa, ambayo yanahitaji uvumbuzi, tung’oe maishani yale mambo ambayo yanaweza sababisha kuanguka na kujaribu tena.
Mwenendo wetu wa Kikristo ni sawa na haya. Maisha ya muumini yanahitaji tuinuke tunapoanguka, tujikung’ute na tuendelee mbele tena. Sio kwamba jambo halikutendeka inamaanisha halitatendeka. Yaweza maanisha tu twahitaji kulitenda tena. Je, mawazo yapi ama majaribio yapi umeyatupilia hapo awali kwa sababu hayakutenda kazi kwa mara ya kwanza…wahitaji kujaribu tena.
Ombi la Leo
Baba wa Mbinguni, nisaidie kukuza tunda la Roho maishani mwangu, hasa matunda ya uvumilivu na kujizuilia. Nifunze kukabiliana na hofu zangu na kutokata tamaa kamwe nikijaribu jambo ulilonipa kutenda.
Maandiko ya Leo
Wafilipi 3:14 nakaza mwendo, niifikilie mede ya dhawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.
Mithali 24:16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
Habakuki 2:3 Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamuriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, ingojee.
Unayemruhusu katika mviringo wako wa ndani anaweza kukuzuilia
Wengi wetu ambao walilelewa na wazazi wamakinifu tulijifunza mapema kiasi ni nani tunapaswa au hatupaswi kumleta nyumbani kumjua mama. Mama walionekana kana kwamba wametengeneza mashine ambayo ingewajuza kama kile kikundi tulichokuwa nacho kama watoto ni kizuri. Walijua kuwa hata tungali watoto, siku zetu za usoni zingeweza kuadhiriwa na ule mviringo wa marafiki na tunapokomaa, ukweli huu hubaki vilevile.
Mviringo wetu wa kati wa marafiki mara nyingi waweza kuwa ndio utatuadhiri sisi zaidi maishani. Wakati mwingi tunawaamini hawa marafiki na kushiriki nao mambo mengi ya siri na ndoto zetu. Pia tunajaribiwa kuwaruhusu kunena zaidi ndani ya maisha yetu. Tunazingatia maoni yao. Hii ndiyo sababu ni muhimu kusikia kutoka kwa Bwana na tuchague kwa umakini uhusiano kulingana na maagizo Yake. Je, unaaminiwa na mviringo wako wa ndani? Wao hukutia changamoto yakutembea juu ya maji ama wanakusababisha kuangalia gharika
kando yako? Pengine unastahili kuwachambua tena watu walio katika mashua yako uone jinsi kila mmoja anavyokuadhiri na utengeze husiano zako vilivyo.
Ombi la Leo
Ewe Mungu, ninakuomba leo unipe mawazo Yako kuhusu marafiki walio maishani mwangu. Ninakuomba unizingire na watu waliojawa imani wenye maono na nia. Ninajua pia ya kwamba mimi ni sehemu ya mviringo wa mtu vilevile, kwa hiyo unitumie niwe adhari nzuri na niwasukumilie karibu na hatua zako kila wakati.
Maandiko ya Leo
1 Wakorintho 15:33 Msidanganyike! Urafiki mbaya huharibu tabia njema.
Matendo ya Mitume 4:23 Mara tu walipoachwa huru, Petro na Yohane walirudi kwa wenzao, wakawaeleza yale waliyoambiwa na makuhani wakuu na wazee.
Mtihani wa kweli wa kuwa mtumishi ni jinsi utakavyofanya wakati utachukuliwa kama mmoja
Watu wengi wangependa kutumika na Mungu lakini sio kila mtu angependa kuandaliwa kwa matumizi. Pia, mara kwa mara, fursa za huduma ambazo Mungu anatupatia zinahitaji ya kwamba tunyenyekee na tuwe watumishi kwa wengine. Yesu alitupa mfano wa kuwa mtumishi wakati alipoyaosha miguu ya wanafunzi Wake. Hii inatuonyesha ya kwamba hakuna aliyee mkuu zaidi hata asifanyike mtumishi na hakuna nafasi iliyo ya juu zaidi ambayo mtu hawezi kuiacha na kutumikia wengine. Ukweli ni kwamba, ukitaka kufanyika mkuu katika Ufalme wa Mungu, ni lazime ufanyike mtumishi kwa wote. Kwahivyo, tutajuaje kama tumemiliki roho ya unyenyekevu na hatujajawa na kiburi na mambo ya kujiona wa muhimu zaidi? Jaribio la kweli la kuwa mtumishi ni vile utakavyofanya ukifanyika kama mmoja. Unajisikiaje unapofanywa kuwatumikia wengine? Ishughulikie.
Ombi la Leo
Baba, ninatamani kuwa na moyo wa utumishi. Unapochagua kunitumia, nitakuwa mtumishi asiyelalamika, nikijua kwamba lolote nifanyalo nitalifanya kama kukufanyia Wewe.
Maandiko ya Leo
Mathayo Mtakatifu 23:11-12 Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu; na yeyeote atakayejikweza, atadhiliwa; na yeyote atakayejidhili, atakwezwa.
Marko Mtakatifu 10:43-45 Lakini kwenu isiwe hivyo, ila anayetaka kuwa mkuu kati yenu, sharti awe mtumishi wenu. Anayetaka kuwa wa kwanza, sharti awe mtumishi wa wote. Maana Mwana wa Mtu hakuja kutumikiwa, ila alikuja kutumikia, na kutoa maisha yake kuwa fidia ya watu wengi."
Kuweza kuwajibika
Huenda ikawa uwezo wetu mkuu ni jinsi tunavyoweza kupatikana, ambapo bila, uwezo wetu wote huenda usitumike. Neno la Mungu linasema ya kwamba tukimwona ndugu anahitaji na tuna suluhisho la kukutana na hilo hitaji, lakini, hatuguswi na huruma ya kusaidia, je, ni vipi upendo wa Mungu unaweza kukaa ndani yetu? Ukiweka kwa njia rahisi, maandiko yanasema ya kwamba kama tuna fursa na uwezo wa kushughulikia hitaji, na bado tunakosa kushughulika, basi uwezo wetu umepotea kwa kukosa kuwajibika.
Wakati watu wengi wanaangalia mamlaka, Mungu anawatafuta watu ambao wanawajibika. Mungu akimpata mtu ambaye anawajibika, ambaye atakayejibu na uweza wake wa kukutana na mahitaji, anawapatia mamlaka yote yanayohitajika kumaliza huduma hiyo. Ni jukumu la Mungu kufungua milango na ni jukumu la mwanadamu kupita kwenye milango hiyo. Jibu wakati unaweza.
Ombi la Leo
Baba, asante kwa kunifanya mimi kuwa zaidi ya kuweza kukumbana na kila changamoto ya maisha na pia uwezo wa kwenda sambamba na kuwasidia wengine katika mahitaji yao pia. Nitajifunza kuegemea mkuu aliye ndani yangu na kukuza hali ya kuwajibika kuhusu kila kitu maishani.
Maandiko ya Leo
Wafilipi 4:13 Nayaweza mambo yote katika Yeye anitiaye nguvu.
1 Wakorintho 10:13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
Ufunuo wa Yohana 3:7 Kwa malaika wa kanisa la Filadelfia andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, ambaye anao ule ufunguo wa Daudi, na ambaye hufungua na hakuna mtu awezaye kufungua.
Usipime kufaulu kwako kwa kila siku
Maisha yamejaa fursa za kufurahisha kupita kiwango na tena fursa za kuhuzunisha kila siku. Wakati mwingine tunajaribiwa kufanya uamuzi kulingana na hisia za wakati huo. Niamini mimi, haijalishi ni nzuri ama mbaya kiasi gani, bado unaweza kuichanganya ama kuiharibu kabisa unapoitenda wakati huo.
Ili uweze kuepuka hali zisizo za kudumu na kutengeneza shida za kudumu, tunahitaji kukataa kuingiliana na tabia za ketenda haraka. Hii inatuhitaji tupunguze mwenendo wa kujibu kulingana na Neno la Mungu na tumpatie Mungu nafasi atusaidie katika mwenendo wa maisha. Usipime kufaulu kwako kwa kila siku.
Ombi la Leo
Baba, nisaidie kuona maisha kupitia macho Yako na kwa mtazamo wako, wala sio mtazamo wnagu. Ninaposhangazwa na kile siku yangu inaleta, nitaweka huko kushangazwa miguuni pako kwa maombi. Nionyeshe jinsi ya kujibu na uniweke salama.
Maandiko ya Leo
Yakobo 1:19 Ndugu zangu wapenzi, kumbukeni jambo hili! Kila mtu na awe mwepesi wa kusikia lakini asiwe mwepesi wa kusema wala mwepesi wa kukasirika.
Mhubiri 5:2 Usiseme maneno ya ujinga kinywani mwako, wala moyo wako usiwe na haraka kunena mbele za Mungu; kwa maana, Mungu Yuko mbinguni, na wewe uko chini, kwa hiyo maneno yako yawe machache.
Mhubiri 7:9 Usifanye haraka kukasirika rohoni mwako, maana hasira hukaa kifuani mwa wapumbavu.
Mithali 19:11 Busara ya mtu huiahirisha hasira yake; nayo ni fahari yake kusamehe makosa.
Wakolosai 3:15 Nayo amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu; maana kwa ajili hiyo ninyi mmeitwa katika mwili huo mmoja. Tena muwe na shukrani!
Mungu haelekezi pale hatatwalia
Moja wapo ya majina ya Mungu katika agano la kale ni Yehova Yire, haswa hili neno limeunganishwa na jina la Mungu kumtambua kwa umakini kama Mtwaliwa wetu. Hata hivyo, maana yake haswa ni, “katika mlima wa Bwana itaonekana”. Baba wetu wa imani, kwanza alimtambua Mungu kama mmoja ambaye atafanya kutwaliwa kupatikane kwa mahali atakapochagua. Kwa hali ya Ibrahamu, Mungu
alimuagiza afunge safari kwa mlima fulani ambapo Ibrahamu alipata kutwaliwa kumemngojea alipofika. Mambo haya hayakunakiliwa katika Biblia kutupasha tu safari ya Ibrahimu, lakini kututia moyo hata nasi katika safari zetu. Wewe, kama Ibrahamu, utapata kutwaliwa kumepeanwa na kuna kusubiri wewe katika kila hali yako mbaya na kwenye safari yako na Mungu. Mungu haelekezi pale hatatwalia. Mtumainie Bwana maana Yeye ni Yehova Yire.
Ombi la Leo
Nionyeshe njia Zako, Eeh Bwana na unipe ufahamu wa barabara unayotaka nipitie. Nielekeze kwa njia yangu iliyoteuliwa, ukinitwalia njiani. Naweka tumaini langu kwako kama chanzo changu.
Maandiko ya Leo
Mwanzo 22:14 Ibrahimu akapaita mahali hapo Yehova-Yire, kama watu wasmavyo hata leo, katika mlima wa Bwana itapatikana.
Warumi 4:1 Tuseme nini basi, juu ya Ibrahimu baba yetu?
Warumi 4:20-24 Ibrahimu hakuionea mashaka ile ahadi ya Mungu; alipata nguvu kutokana na imani, akamtukuza Mungu. Alijua kwamba Mungu anaweza kuyatekeleza yale aliyoahidi. Ndiyo maana Mungu alimkubali kuwa mwadilifu. Inaposemwa, "Alimkubali," haisemwi kwa ajili yake mwenyewe tu. Jambo hili linatuhusu sisi pia ambao tunamwamini Mungu aliyemfufua Yesu, Bwana wetu, kutoka wafu.
Mungu hakukusudia uhusiano wake na mwanadamu kuchukua nafasi ya uhusiano wa mwanadamu na mwingine
Katika kitabu cha Mwanzo, Mungu alimuumba binadamu kwa mfano wake mwenyewe na kumuweka kwenye shamba. Baadaye Mungu akatazama yale yote aliyokuwa amefanya na akaona jambo moja ambalo halikuwa zuri. Akasema, “Sio vizuri kwa mwanadamu kukaa peke yake.” Kwa hivyo Mungu akamuumba mwanamke.
Ijapokuwa hakuna kina kinachoweza kubadilishana uhusiano wako na Mungu, Mungu hakukusudia uhusiano Wake na wewe kuchukua nafasi ya uhusiano wako na mtu mwingine. Anajua kwamba watu wanahitaji watu. Tunahitajiana mmoja nao mwingine. Tumia wakati leo katika uhusiano huo wa muhimu katika maisha yako…pamoja na Mungu na wapendwa wako.
Ombi la leo
Bwana, nataka uhusiano wa kina wewe. Wewe ni wa muhimu sana maishani mwangu. Kwa wakati huohuo, nataka kujenga na kufurahia uhusiano ulionipa na watu wengine. Nisaidie kujua na kufuata kipaumbele katika uhusiano wangu. Asante.
Maandiko ya Leo
Mwanzo 2:18 Bwana Mungu akasema, si vema huyu mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Waefeso 5:31 Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: "Kwa hiyo, mwanamume atawaacha baba na mama yake, ataungana na mkewe, nao wawili watakuwa mwili mmoja."
Mithali 18:24 Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.
Mabadiliko yanakuja – upende usipende, mabadiliko yanakuja Mabadiliko huenda yakawa ni baadhi ya mambo yasiyotulia na wakati wa kushusha sana maishani. Kutoka mahali pamoja hadi pengine, kazi moja hadi nyingine, ama majira haya ya maisha hadi mengine, ni ukawaida wa maisha. Sio mabadiliko yote ni mabaya, na wakati mwingi mabadiliko ni ya muhimu na hayaepukiki.
Imeshasemwa ya kwamba Mungu anatupenda sana hata hawezi kutuacha jinsi tulivyo. Jambo moja ni la hakika, mabadiliko yanakuja, upende usipende, mabadiliko yanakuja kwako. Ukikumbana na mabadiliko maishani, kuwa mwepesi wa kubadilika, mwamini Mungu, na upate maono ya siku kuu.
Ombi ya Leo
Mungu, nifunze kukumbatia nyakati za mabadiliko ambayo ni muhimu na haziwezi kuepukika maishani. Niongoze kupitia kutokuwa na uhakika kwangu na hali ya kujishuku na unipe maono Yako ya siku bora kwa upande mwingine wa mabadiliko.
Maandiko ya Leo
Wafilipi 3:13-14 Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kishika; ila natenda neneo moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; nakaza mwendo, niifikilie mede ya dhawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu.
Isaya 43:19 Tazama, nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je! Hamtalijua sasa? Nitafanya njia jangwani, na mito ya maji nyikani.
Mungu anakutengenezea siku za usoni na anatengeneza “wewe” kwa siku hizo za usoni Maandiko yanatufunilia ya kwamba Mungu amejitoleakuendelea kufanya kazi nasi, kama vile mfinyanzi anafanya kazi na udongo. Yeye anakumbana na kila jukumu la kila siku na kila hali ya maisha kuleta kila mmoja wetu katika mfnao wa Mwanawe wa pekee, Bwana wetu na Mwokozi, Yesu.
Mungu anatengeneza siku za usoni kwako; halikadhalika anaumba uweza mkuu ndani yako wa kukumbatia siku za usoni. Ni kwa sababu hii Mungu ameamuru mambo yote kutendeka kwa wema wetu. Na ameunda misukumo ya maisha kutufanya kuwa bora, lakini sio watu wa machungu. Kumbatia mfano ulio bora na uanze kujiona vile Mungu anavyokuona. Ota ndoto zake maishani mwako na uwache akuumbe upya.
Ombi la Leo
Mungu, Baba yangu, nijenge mimi na unipe milki…nipeleke katika siku za usoni ulizoniotea uliponiumba. Nisaidie niwe wa kujengeka kuumbika katika mikono Yako. Fanyika kuwa mfinyanzi mkuu nami nitakuwa udongo. Nifanye wa kufurahisha mbele zako.
Maandiko ya Leo
Wafilipi 1:6 Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba Yeye aliyeanza kazi njema ndani yenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu.
Zaburi 138:8 Bwana atanitimilizia mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; usiziache kazi za mikono yangu.
1 Timothy 4:8 Mazoezi ya mwili yana faida yake, lakini mazoezi ya kiroho yana faida za kila namna, maana yanatuahidia uzima katika maisha ya sasa, na pia hayo yanayokuja.
Isaya 64:8 Lakini sasa, Ee Bwana, wewe u Baba yetu; sisi tu udongo, nawe u mfinyanzi wetu; sisi sote tu kazi ya mikono yako.
Jifunze kukimu makabiliano badala ya kuyaepuka kila wakati Makabiliano mara nyingi ni hatua ya muhimu kuelekea kuwa na umoja. Ni mara nyingi kwenye mng’ang’ano tunauafikia uamuzi ulio bora nakufika kwenye makubaliano wakati yaliyo bora yametambulika. Usiendelee kupitia maisha ukiogopa kukabiliana ya kwamba utashindwa kutambua dhamana na manufaa ya
makabiliano. Sio lazima tu tung’ang’ane na maadui zetu, lakini pia tuwatie nguvu marafiki wetu, tupanue uhusiano wetu, na tutafute majibu ambayo hayajavumbuliwa kwa changamoto za maisha. Tungelikuwa wapi sisi sote pamoja kama tungewachilia mbali misukumo, ming’ang’ano, na ugumu wa kuzaa mtoto? Kumbuka, la muhimu linapatikana wakati ambapo tunang’ang’ana tukitafuta ukweli, kando na makabiliano. Jifunze kikimu makabiliano badala ya kuyaepuka kila wakati.
Ombi la Leo
Baba, nifunze kusimama imara, kutokuogopa makabiliano ya maisha haya. Nipe neema ya kukimu muda wakati mng’ang’ano ni muhimu kufikia kilele changu kwako. Usiruhusu makabiliano yalete mgawanyiko lakini nitendeshe kazi mimi ili niwe na nguvu katika Jina la yesu.
Maandiko ya Leo
Mithali 27:17 Chuma hunoa chuma; ndivyo mtu anunoavyo uso wa rafiki yake
1 Petro 4:12 Wapenzi wangu, msishangae kuhusu majaribio makali mnayopata kana kwamba mnapatwa na kitu kisicho cha kawaida.
2 Wakorintho 4:18 Hivyo tunatazamia kwa makini si vitu vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Maana vinavyoonekana ni vya muda tu; lakini vile visivyoonekana ni vya milele.
Baraka zetu kuu maishani huenda ikawa zinatungojea tuwe wa baraka kwa wengine Hadithi ya Ayubu, hata pia hadithi ya Yusufu, zote ni mwelekeo ya kanuni hii ya kiungu maishani. Yusufu hangelipata kuachiliwa kutoka korokoroni kama hangelichukua muda kuwa mkarimu na wa baraka kwa yule mkuu wa kubeba kikombe cha Farao alipokuwa gerezani. Hata hivyo, Ayubu alijipata mahali maishani ambapo alipoteza kila kitu. Katika sura ya mwisho iliyonakiliwa kwa hesabu za Ayubu, tunasoma ya kwamba Bwana aligeuzwa utumwa wake wakati Ayubu alwaombea marafiki wake.
Hata Mungu hakujitoa katika kanuni ya ukweli huu. Unaona wakati Mungu alikuwa ametengwa kutokana na maumbile yake, na mwanadamu alikuwa anaeleka kuzimu, Mungu alikuwa na njia moja tu ya kufikia shauku Yake kuu. Ni nini ambayo ingembariki Mungu? Ilikuwa ni kurudi kwa uhusiano sawa na mwanadamu. Hata hivyo, urejesho ulihitaji dhabihu. Ili Mungu abarikiwe, ilimbidi kwanza awabariki wengine. Kwa hivyo Mungu akamtuma Mwanawe wa pekee na akambariki mwanadamu kwa msamaha wa dhambi, na baadaye Mungu
akabarikiwa na watoto wengi. Baraka zetu kuu maishani huenda ikawa zinatungojea tuwe wa baraka kwa wengine.
Ombi la Leo
Baba Mpendwa wa Mbinguni, nauliza Roho Wako Mtakatifu anikumbushe katika lisaa langu kuu la hitaji ya kwamba wengine pia wameketi kwenye mahitaji. Nisaidie nitazame tena maisha yangu ili niwe wa baraka kwa wengine ninaposubiri baraka zako kwenye maisha yangu na kazi.
Maandiko ya Leo
Waefeso 6:8 Kumbukeni kwamba kila mtu mwenye kutenda mema, awe mtumwa au mtu huru, atapokea tuzo lake kutoka kwa Bwana.
Mwanzo 12:2 Nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka.
Wagalatia 6:7 Msidanganyike; Mungu hafanyiwi dhihaka. Alichopanda mtu ndicho atakachovuna.
Wale hawataondoka hawatabanduka Maisha yamejaa mabadiliko…mambo yanaanza na mambo yanaisha. Mara nyingi tukifikia mwisho huu tunatambua ni kuanza safari kwa hatua nyingine kuu ya shani zetu. Wakati mwingine Mungu anatutuma kwenye barabara fulani kufika mwisho wa barabara hiyo na wakati mwingine Mungu anatuelekeza kwenye barabara hiyo kufika kwenye njia panda. Kwa hali zote mbili mabadiliko yanahitaji uamuzi wa ujasiri na kujitolea rasmi.
Wakati mwingine maisha yanatuhitaji tuachilie jambo moja kabla hatujashika lingine. Kuachilia siku zilizopita maramara haisawazishwi na kuachilia watu wa siku zilizopita. Wakati mwingi, inatubidi tu tuachilie siku zilizopita kwa kusamehe kuumizwa kwa roho, kushushwa, na kuanguka. Hata hivyo, kuna nyakati ambazo zitatuhitaji kujitenga kikamilifu kutokana na mtu binafsi ama kikundi cha watu kabla hatujakumbatia siku mpya ambayo Mungu anataka kwa ajili yetu. Kuondoka ni nadra lakini mara kwa mara kabla ya kubanduka, inawezekana.
Ombi la Leo
Bwana, ninaelewa ya kwamba ni lazima niwachilie baadhi ya mambo ili niyashike mengine. Nionyeshe jinsi ya kufanya hivyo. Ninataka kukufurahisha Wewe zaidi ya chochote ama mtu yeyote. Nipe hekima ya kupambanua kinachohitajika katika mafikira yangu maishani mwangu. Nitafuata hekima yako.
Maandiko ya Leo
Waefeso 4:22-24 Basi, acheni mwenendo wenu wa awali, yaani ule utu wenu wa kale uliokuwa unaangamizwa kwa tamaa zake danganyifu. Jirekebisheni upya rohoni na katika fikira zenu. Vaeni hali mpya ya utu ambayo imeumbwa kwa mfano wa Mungu na ambayo hujionyesha katika maisha ya kweli ya uadilifu na utakatifu.
Mwanzo 2:24 Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
Mathayo 19:5 … na akasema: “Kwa sababu hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake, ataungana na mke wake, nao wawili watakuwa mwili mmoja”
Wakati mwingine msimu wetu wa maisha hututaka tumtumainie Mungu katika wengine
Katika Mwanzo 22 Ibrahimu aliambiwa amtwae mwanawe Isaka hadi mahali Mungu angemwonyesha na amtoe kama thabihu kwa Mungu. Wakati huu isaka alikuwa na miaka kati ya 30 na 35. Ibrahimu alimchukua isaka na kutembea kwa siku tatu kaskazini mwa Barsheba hadi mahali ambapo hivi leo ni mji wa kale wa Yerusalemu. Ibrahimu aliweka kuni za thabihu kwenye mabega ya Isaka na wakaushuka mlima ambao Mungu alimwonyesha Ibrahimu. Hadithi inaendelea ambapo Ibrahimu akimfunga mwanawe kwa kamba, akiweka kuni katika madhabahu mapya na kumweka isaka tayari kumtoa kama kama dhabihu. Waebrania 11 inasema kuwa Ibrahimu alimtumainia Mungu… lakini Isaka alimtumainia nani?
Isaka alimhoji babake na akasikia jibu la babake kisha akamkubali babake amfunge na kumtayarisha ili amtoe kama dhabihu. Katika haya yote Isaka alimtumainia Mungu katika Ibrahimu ingawa Isaka hakusikia kwa uhalisi kutoka kwa Mungu. Wakati mwingine misimu yetu na hali zetu za maisha hututaka tumtumainie Mungu katika wengine.
Ombi la leo.
Ewe baba wa Mbinguni, nisaidie kupambanua nyakati na misimu ya maisha inayonitaka nikutumainie katika na kupitia zingine. Nipe neema ya kukubali uongozi unaonitumia na nikakubali uniongoze katika nyakati hizi kulingana na mapenzi yako.
Maandiko ya leo.
Mwanzo 22:7-9 Isaka akasema na Ibrahimu baba yake, akinenea, Babangu! Naye akasema, Tazama! Moto upo, na kuni zipo, lakini yuko wapi mwana-kondoo kwa sadaka ya kuteketezwa? Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-
kondoo kwa hiyo sadaka,mwanangu. Basi wakaendelea wote wawili pamoja. Wakafika mahali pale alipoambiwa na Mungu, Ibrahimu akajenga madhabahu huko, akziweka tayari kuni, kasha akamfunga Isaka mwanawe, akamweka juu ya madhabahu, juu ya zile kuni.
Waebrania 11:17 Kwa imani, Ibrahamu alimtoa mwanae Isaka sadaka wakati Mungu alipomjaribu. Huyo Abrahamu ndiye aliyekuwa amepokea ahadi ya Mungu, lakini, hata hivyo, alikubali kumtoa dhabihu mwanae wa pekee,
Sio kila wakati kila aliyeadhirika husikia kutoka kwa Mungu
Kama tulivyojadiliana katika funzo la jana, Ibrahimu alisikia kutoka kwa Mungu eti amtoe mwanawe Isaka kama dhabihu… Isaka alisikia kutoka kwa Ibrahimu tu. Hatuna njia ya kujua kama isaka alisikia sauti kutoka mbinguni ikimwambia Ibrahimu abadilishe mipango yake na asimtoe mwanawe Isaka kama dhabihu. Hata hivyo kuna matukio mengine mengi ambapo si kila aliyeathirika alisikia kwa uhalisi kutoka kwa Mungu. Hivyo ndivyo ilivyokuwa katika kisa cha Samweli ambaye akiwa mvulana mdogo alisikia sauti ya Mungu ikiliita jina lake na kunena ujumbe ilhali Eli kuhani mzee hakusikia.
Mungu humnenea anayetaka na wakati mwingine si kila aliyeathirika kwa sauti hiyo huisikia sauti hiyo. Mruhusu Mungu achague yule anayetaka kutumia, na bila shaka wakati mwingine utasikia kutoka kwa Mungu; na wakati mwingine utasikia kutoka kwa wengine ambao Mungu amewachagua kunena.
Ombi la leo.
Ewe Baba wa Mbinguni, nipe neema ya kukutumainia ninaposikia ukinizungumzia na pia nikutumainie kupitia uongozi wa wengine uliowaweka maishani mwangu. Ninajua sauti yako haiwezi kukiuka Neno Lako. Nifunze Neno Lako Ewe Bwana.
Maandiko ya leo.
1 Samweli 3:9, 10, 11, 15 Kwa hivyo, Eli akamwambia Samweli, Enenda, kalale; itakuwa, akikuita, utasema, Nena Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Basi Samweli akaenda akalala mahali pake. Bwana akaja, akasimama, akaita vile vile kama kwanza, Samweli! Samweli! Ndipo Samweli akasema, Nena, Bwana; kwa kuwa mtumishi wako anasikia. Bwana akamwambia Samweli, Angalia, nitatenda tendo katika Israeli, ambalo kila atakayelisikia masikio yake yatamwasha. Naye Samweli akalala hata asubuhi, akaifungua milango ya nyumba ya Bwana. Samweli akaogopa kumjulisha Eli maono hayo.
Usiwahi kudunisha nguvu za maono
Mara nyingi watu huacha kuona siku zao za usoni kwa sababu ya hali wanayopitia. Wingu la kuchanganyikiwa na misimu ya kufadhaika hufanya kazi ya kutunyang’anya tumaini letu kwa ajili ya siku zetu za usoni. Katika nyakati hizi za kuchanganyikiwa hakuna kitu kitakachonyoosha maisha kama kuwa na maono kwa siku kuu. Hata kama tunakumbana na jaribio gumu maishani au kupitia
mabadiliko ya misimu ya maisha, tumaini kwa siku za kesho zilizo bora zaidi ndio ufunguo wa sisi kusonga mbele kwa mwito ulio imara. Usikubali uvuli wa wakati ukufungie katika wakati huo. Angalia mbele na umuulize Mungu akupe maono ya kesho kama alivyokupangia.
Usiwahi kudunisha nguvu za maono. Itakurejeshea furaha, ikupe nguvu, na ikuongoze katika mabonde ya maisha. Usisahau, siku yako kuu zaidi ingali mbele.
Ombi la leo.
Ewe Mungu, ninaomba unipe maono ya yale umenipangia katika siku zangu za usoni. Nitembelee wakati wangu wa usiku na uninenee kwa kupitia maono na ndoto. Nitie nguvu na unipe furaha unaponiongoza kwa ukuu wangu kwa roho wako mtakatifu.
Maandiko ya leo.
Zaburi 126:1 Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni, tulikuwa kama waotao ndoto.
Ayubu 33:14-16 Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali. Katika ndoto, katika maono ya usiku, usingizi mzito uwajiliapo watu, katika usingizi kitandani; ndipo huyafunua masikio ya watu, na kuyatia muhuri mafundisho yao.
Matendo ya Mitume 2:17 `Katika siku zile za mwisho, asema Bwana, nitawamiminia binadamu wote Roho wangu. Watoto wenu, wanaume kwa wanawake, watautangaza ujumbe wangu; vijana wenu wataona maono, na wazee wenu wataota ndoto.
Mithali 29:18 Pasipo maono, watu huacha kujizuia; bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Mungu ni Mungu wa “nitumainie, nijaribu, na unithibitishe”
Mungu ni wa umilele, si mwenye nguvu zote tu, bali wa umilele. Mungu hawezi kutiwa majaribuni au hawezi kushawishiwa kujibu maswali yetu. Ilhali amejitolea kujithibitisha kwa wana wake ili tuwe na ujasiri mkubwa katika neno lake na tuongeze imani yetu kwake. Kupitia chaguo kuu la Mungu amesema kuwa tunaweza kumjaribu na tuone kama hatatenda neno lake kwa niaba yetu.
Andiko moja kama hili katika Malaki hushughulikia zaka na sadaka zetu. Amua leo kuwa utamtumainia Mungu umjaribu na umkubali athibitishe uaminifu wake kwa niaba yako. Inaanza unapotumia neno la Mungu katika hali zako za maisha. Mjaribu leo.
Ombi la leo.
Bwana, wewe pekee ndiwe Mungu na hakuna mwingine kando na wewe. Asante kwa kunipenda na kunijali. Katika mambo yote nitakutumainia kupitia kwa neno lako. Nionyeshe unachotaka nifanye nami nitafanya. Imani yangu ikuavyo, nifunze kushiriki shuhuda hizo na wengine.
Maandiko ya leo.
Malaki 3:10 Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi; mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
Zaburi 9:10 Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe, maana Wewe, Bwana, hukuwaacha wakutafutao.
Zaburi 56:11 Nimemtumaini Mungu, sitaogopa; mwanadamu atanitenda nini?
Kama Mungu si namba moja katika siku yako, yawezekana yeye si namba moja maishani mwako.
Maisha yana shughuli nyingi na siku hujazwa haraka na majukumu yanayotumia muda wetu. Siku hupita na kugeuka kuwa majuma na majuma kuwa miezi kabla tugundue. Mara nyingi inaonekana kuna wakati mdogo wa kutulia na kufurahia mambo madogo ya maana ya maisha.
Tusipokuwa waangalifu, uhusiano wetu na Mungu unaweza kuwa moja ya zile zitakazoumia. Ni rahisi sana kumzima, kulegea katika tabia zetu za maombi na kupatia masomo ya Neno la Mungu mahali pake sawa katika siku yetu. Hata hivyo, kama Mungu si namba moja katika maisha yako yaweza kujadiliwa kuwa huenda ikawa yeye si namba moja maishani mwako. Fanya mabadiliko sasa. Weka nadhiri ya kuanza kila siku na Mungu.
Ombi la leo.
Baba, nisamehe pale ambapo sikukujumulisha katika wakati muhimu wa siku yangu. Nikumbushe kila asubuhi ya kuwa unaningoja nitumie wakati wako nawe. Fungua hazina za ufalme wako kwangu tunapoangalia neno lako pamoja. Sikia ombi langu, ewe Mungu. Ninakupenda.
Maandiko ya leo.
Mwanzo 19:27 Ibrahimu akatoka asubuhi kwenda mahali aliposimama , mbele za Bwana.
Marko 1:35 Kesho yake, kabla ya mapambazuko, Yesu alitoka, akaenda mahali pa faragha kusali.
Mithali 8:17 Nawapenda wale wanipendao na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
Msaada mara nyingi uko hatua moja tu ya uamuzi mgumu
Nimesikia inasemekana kuwa kama pesa zinaweza kuitengeneza, wakati waweza kuitengeneza, ama kama ni uamuzi mgumu, si shida bali ni fursa. Hata hivyo kuna hali zingine ambazo zaweza kutatuliwa tu kwa kufanya uamuzi ambao ni mgumu kufanya. Hii ndiyo iliyokuwa hali ya Mungu alipokumbana na hali ya kutengana milele na wanadamu. Hakuna kiasi cha pesa ambacho kingesuluhisha na wakati bila suluhisho ungefanya hali hiyo ngumu zaidi. Suluhisho pekee la shida ya Mungu lilikuwa kumtuma mwanawe kama mtoto, akazaliwa katika hori la ng’ombe kule Bethlehemu, hatima yake ikiwa kukataliwa, kuumizwa, kuchapwa, na kusulubiwa, yote hayo kwa dhambi ambazo hakufanya. Huu ulikuwa uamuzi mgumu lakini hakukuwa na msaada na hakuna mwingine ambaye angeufanya uamuzi huu ila Mungu. Ingawa hakuna kafara nyingine itahitajika, tunakumbana na hali ambazo haziwezi kutatuliwa bila ya sisi kufanya uamuzi mgumu. Kubali ukweli, msaada mara nyingi uko hatua moja tu ya uamuzi mgumu ... na huenda ukawa ni wewe pekee unayeweza kuisuluhisha.
Ombi la leo.
Ewe Bwana, nisaidie kuchukua jukumu langu kwa kumaanisha na nifahamu kuwa kuna vitu vingine ambavyo mimi tu ndiye ninayeweza kusuluhisha. Nisaidie kukumbana na kufanya uamuzi ufaao hata kama ni mgumu.
Maandiko ya leo.
Isaya 53:3-5 Alidharauliwa na kukataliwa na watu; mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, alidharauliwa na wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, amejitwika huzuni yetu; lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa makos ayetu; adhabu ya amni yetu ilikuwa juu yake, na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.
Kumbukumbu la Torati 30:19 Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako.
Mungu huwapa watu kupitia watu
Usiku kabla ya Krismasi Mungu alikuwa ameshajitayarisha kupeana zawadi yake kuu… zawadi ya wokovu. Mungu alichagua vipi kuipeana zawadi yake kuu? Alichagua kuuleta wokovu kwa wanadamu kupitia Yesu wa Nazareti. Mara nyingi Mungu anapotaka kazi ifanywe mwana huzaliwa. Kwa nini? Kwa sababu Mungu amechagua kuwapa watu kupitia watu. Hata kama Yesu ni Mwana wa Mungu yeye pia ni mwana wa mwanadamu na ni kupitia kwa utu wake ndiyo Yesu alilipa deni na kuleta zawadi ya Mungu.
Kanuni hii yaendelea kupitia maandiko na maisha. Kama Mungu anatamani kukubariki yeye mara nyingi huchagua kutuma Baraka hizo kupitia mtu mwingine. Unaona, Mungu mara nyingi hawezi kukupa kile hawezi kupeana kukupitia. Mungu anataka kuwabariki wengine leo… anaweza kukutumaini? Je Mungu akikubariki utawabariki wengine? Wacha Mungu ajue kuwa u tayari kupeleka zawadi yake kwa mtu mwenye hitaji leo.
Ombi la leo.
Mungu, ninakushukuru kwa Mwanao Yesu na kwa zawadi ya wokovu aliyoniletea. Nitumie, Bwana, kuwasilisha zawadi yako kwa wengine wanaoihitaji. Nibariki na unifanye niwe baraka. Nipe na unitumie kuwapa wengine katika jina la Yesu. Amina.
Maandiko ya leo.
Luka 6:38 Wapeni wengine wanavyohitaji, nanyi mtapewa. Naam, mtapokea mikononi mwenu kipimo kilichojaa, kikashindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika. Kwa maana kipimo kilekile mnachotumia kwa wengine ndicho ambacho Mungu atatumia kwenu."
Mwanzo 12:2 Nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka
Luka 19:8 Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, "Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang`anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne."
Mapenzi ya Mungu kwako ni mazuri.
Hivi leo, Wakristo wengi husherehekea kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu, Masihi wa Wayahudi na Mwokozi wa ulimwengu. Usiku ambao Yesu alizaliwa malaika waliwatokea wachungaji katika viwanja vya Bethlehemu wakitangaza mapenzi ya Mungu kwa ulimwengu uliopotea na unaoumia. Juu ya haya yote usiku huo mzuri kulikuwa na ufunuo ulioletwa na malaika kwa wanadamu. Malaika waliimba, “amani duniani na mapenzi ya Mungu kwa wanadamu.”
Ingawaje siwezi kukuambia Mungu amekuwekea nini au njia anayoweza kukuongoza, ninaweza kutangaza kuwa mapenzi ya Mungu kwako ni mazuri. Hana hasira, Hamtakii yeyote mabaya au kuwa na wivu kwa mwanadamu. Yesu, Mwana wake, aliyezaliwa na bikira katika mji wa Bethlehemu alionyesha ulimwengu kuwa kile Mungu anatutakia ni kwa uzuri wetu. Mtumainie huyu Mungu mzuri na mpango wake mzuri kwa maisha yako kwa kumkubali huyu Yesu kama Bwana na Mwokozi.
Ombi la leo.
Ewe Baba wa Mbinguni, leo ninakushukuru kwa kumtuma Mwanao Yesu duniani. Ninaamini alizaliwa na bikira, akaishi maisha yasiyo ya dhambi, na akafa kifo cha uchungu na aibu. Ninaamini kile malaika walitangaza na ninaweka nadhiri kuwa nitawaeleza wengine habari hii njema.
Maandiko ya leo.
Luka 2:10-14 Malaika akawaambia, "Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote. Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana. Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini." Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema: "Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!"
Msamaha wa dhambi si kibali cha dhambi
Yesu, Mwana wa Mungu, Masihi wa Wayahudi na Mwokozi wa Ulimwengu alizaliwa na bikira katika mji wa Bethlehemu, aliishi maisha yasiyo na dhambi na kufa kifo cha uchungu na aibu. Dhabihu yake msalabani Kalvari ililipa milele dhambi za wanadamu. Yesu alikufa kuokoa roho zetu kutoka kuzimu ya milele na kutokana na kuzimu ya maisha haya. Alitukomboa kutokana na nguvu ya dhambi ya kuangamiza roho zetu milele na kutokana na nguvu za dhambi za kutawala maisha yetu kwa muda. Msamaha wa Mungu kupitia damu ya Yesu, ikitumika mara moja, imekamilika. Hakumbuki dhambi zilizosamehewa; anazitupilia nyuma yake; anaziangusha katika bahari la sahau; na kuzitoa zetu kama vile mashariki ilivyo mbali na magharibi. Mungu baba, alimwekea Yesu, Mwana, makosa yetu yote na tumesamehewa. Hata hivyo, msamaha wa dhambi si kibali cha kutenda dhambi.
Ombi la leo.
Baba, watu wote wamefanya dhambi na kupungukiwa na utukufu wako na mshahara wa dhambi ni mauti bali karama yako ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. Nisamehe dhambi, nioshe kutokana na kutokuwa mwenye haki na unipe neema yakutembea huru kutokana na mshiko utawala wake.
Maandiko ya leo.
Warumi 6:14 Maana, dhambi haitawatawala ninyi tena, kwani hamko chini ya Sheria, bali chini ya neema.
Warumi 10:13 Maana Maandiko Matakatifu yasema: "Kila mtu atakayeomba kwa jina la Bwana, ataokolewa."
Isaya 53:6 Sisi sote kama kondoo tumepotea; kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe; na Bwana ameweka juu yake maovu yetu sisi sote.
Zaburi 25:11 Ee Bwana, kwa ajiliya Jina lako, unisamehe uovu wangu, maana ni mwingi.
Isaya 55:7 Mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie Bwana, naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.
Ulichofanya kupata kitu ndicho unachohitaji kufanya kwa ujumla ili ukiweke
Yohana alipoandika kitabu cha Ufunuo, Yesu alimnenea kuhuhu Kanisa la Efeso. Hili lilikuwa kanisa zuri lililofanya kazi, lilikuwa na mazao, lilikuwa na uvumilivu, lilichukia maovu, na lilichunga dini. Yote haya waliyafanya bila kuchoka kwa ajili ya Yesu na Jina Lake. Hata hivyo, Yesu alikuwa na jambo moja dhidi yao: walikuwa wameuacha upendo wao wa kwanza. Je, Yesu alikuwa akizungumzia nini? Alikuwa akisema kanuni ambayo misingi ya Kikristo haitabadilika na haijalishi tuna mazao kiasi gani ama tunahusika kiasi gani kama tumeunganishwa kwa mtiririko wa maisha wa uhusiano unaotokana na uhusiano wa ndani na yesu, kazi zetu zote ni bure. Ni sawa na kila uhusiano, hata ndoa na/au kazi yako. Ulichofanya kupata kitu ndicho unachohitaji kufanya kwa ujumla ili ukiweke. Rudi kwa misingi na usiusahau upendo wako wa kwanza.
Ombi la leo.
Baba Mungu, nionyeshe makosa na motisha ya kweli ya moyo wangu. Nisaidie nisiusahau upendo wangu wa kwanza na nilichofanya ili nifike nilipo. Nifunze kudhamini misingi ya maisha na uhusiano ninapoendelea kuutumikia Ufalme wako.
Maandiko ya leo.
Ufunuo wa Yohana 2:1-5 "Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: "Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu. Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo. Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo. Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali. Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.
Hakuna awezaye kupewa kamili hadi avunjike kamili
Mungu huwapinga wajikuzao bali huwapa neema wanyenyekevu. Unyenyekevu ni kujua kila wakati kuwa tunamtegemea Mungu. Mara nyingi katika injili zote, Yesu anaonekana akitwaa mkate, akiubariki kisha kuumega kabla ya kuupeana. Kanuni hii inatunenea kuhusu mpangilio wa Mungu maishani mwetu. Mkono wa thamani wa Mungu utuchukuao na kutusongeza karibu naye ndio mkono wa upendo unaotubariki. Kwa watu wengi huu ndio umbali watakaomkubali Mungu kuhusiana nao. Hata hivyo ili upewe kamili yafaa umruhusu Mungu huyo anayejali aingie ndeni ya kina cha maisha yako. Anajua kilicho ndani ya mwanadamu na anajua unachoweza. Mungu anataka kukuchukua na anataka kukubariki lakini anataka kukuvunja ili upeanwe. Wale wawili njiani wakielekea Emau walitoa ushuhuda kwa wanafunzi wengine wakisema, “tulimtambua katika kuumega mkate.” Usife moyo Mungu anapoanza kushughulikia kiburi chako au dhambi zingine kuu maishani mwako. Makusudi yake ni kukupeana.
Ombi la leo.
Ewe Bwana, kuwa mwenye rehema kwangu na ukumbuke mimi si kitu ila vumbi tu. Usinipige kwa kutoridhika kwako, lakini chukua maisha yangu, bariki maisha yangu, vunja maisha yangu katika mikono Yako miepesi, unapopenda, ili unipeane kama unavyohitaji katika jina la Yesu. Amina.
Maandiko ya leo.
Yohana 2:25 … Hakuhitaji kuambiwa chochote juu ya watu, maana aliyajua barabara mambo yote yaliyomo mioyoni mwao.
Luka 24:35 Basi, hao wafuasi wawili wakawajulisha yale yaliyowapata njiani, na jinsi walivyomtambua katika kumega mkate.
Mathayo 26:26 Walipokuwa wanakula, Yesu akatwaa mkate, akashukuru, akaumega, akawapa wanafunzi wake akisema, "Twaeni mle; huu ni mwili wangu."
Yakobo 4:6 Lakini, neema tunayopewa na Mungu ina nguvu zaidi; kama yasemavyo Maandiko: "Mungu huwapinga wenye majivuno lakini huwapa neema wanyenyekevu."
Kama ni mbaya Mungu hajamaliza bado
Waweza kuwazia, kutokana na mtazamo wa binadamu, jinsi ilivyoonekana vibaya kwa Yesu alivyotazama msalaba kuadhibiwa kwa makosa ambayo hakutenda? Hakika, alinakiri kutoka Zaburi 22 alipoangikwa msalabani akisema, “Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?” Yusufu huenda alikuwa na hisia hizo wakati mwingi na hata pia Ayubu, Paulo, Petro, Mariamu na watakatifu wengine wengi katika Biblia.
Kumbuka, imani ni kuamini ya kuwa haijalishi tuliko au tunakabiliana na nini maishani, Mungu yu kwenye usukani. Chukua nguvu na imani leo kutoka kwa hadithi za watakatifu waliothihirishwa kwetu katika Maandiko na ujue kama ni mbaya Mungu hajamaliza bado!
Ombi la leo.
Mungu, nisaidie kugundua kuwa Hakuna lilio gumu kwako. Ninajua kuwa maisha yangu na wakati wangu u kwako na mazuri yangali yaja!
Maandiko ya leo.
Warumi 8:28 Tunajua kwamba, katika mambo yote, Mungu hufanya kazi na kuifanikisha pamoja na wote wampendao, yaani wale aliowaita kufuatana na kusudi lake.
Yohana 16:33 Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!"
Mungu huzungumza kupitia hatima
Mungu alipomwambia Musa kuwakomboa wanawe kutoka bonde la Misri, alimtuma Musa na ujumbe kutoka mbinguni. Ujumbe Musa alionena kwa niaba ya Mungu kwa wana wa Israeli ulikuwa sambamba kabisa: “Nitawakomboa kutoka Misri na kuwapeleka katika nchi ya ahadi ya maziwa na asali.” Mungu alipomtuma nabii Samweli kumpaka mafuta kijana mdogo Daudi ili awe mfalme wa Israeli yote, alimnenea Daudi kupitia nabii kuhusu hatima yake kuu ya kuwatawala wana wa Mungu. Yesu alipokutana na wanafunzi wake wa kwanza ufuoni mwa Galilaya aliwaita kwa kuwaambia, “Njooni mnifuate nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.”
Maneno haya yote ya Mungu yanawanenea wanadamu kuhusu hatima bila kuashiria safari ndefu, ngumu na inayogharimu ili mtu afike hatima ile. Mungu hutunenea kuhusu hatima, kisha hutembea nasi safarini tukielekea hatima hiyo. Maisha ni safari…na ukiwa na Mungu safari ni rafiki yako.
Ombi la leo.
Mungu, nipe hekima ya kukubali mapenzi yako kwa maisha yangu na nguvu za kutembea njia yako kwa mapenzi hayo. Amina.
Maandiko ya leo.
Wagalatia 6:9 Basi, tusichoke kutenda mema; maana tusipolegea tutavuna mavuno kwa wakati wake.
Hesabu 21:4 Wakasafiri kutoka mlima wa Hori kwa njia ya Bahari ya Shamu; ili kuizunguka nchi ya Edomu, watu wakafa moyo kwa sababu ya ile njia.
Mathayo 4:19 Basi, akawaambia, "Nifuateni, nami nitawafanya ninyi wavuvi wa watu."
Siku yako kuu haitakuja hadi ushinde jaribio lako kuu
Kama ilivyo na kuzaliwa kwa kila kitu, kuanzia wanadamu, kupitia ufalme wa wanyama, na hata mbegu tunazopanda, maisha huanza kwa mng’ang’ano. Siku baada ya siku, mwaka baada ya mwaka, maisha huendelea kutiwa nguvu tunaposukuma kinyume na nguvu zinazopinga ukuaji wetu na kujaribu kutushikilia nyuma. Mng’ang’ano ni sehemu ya maisha inayoendelea kwa maana ni kupitia kwa mng’ang’ano ndipo tunatiwa nguvu. Yakobo aling’ang’ana na malaika, Paulo na mambo yake ya kale, na Yesu na hatima yake. Katika kila mng’ang’ano wake kwa waume walioshinda na kunyakua ushindi katika hali hizo ni wale ambao pia wanaenda mbele na kunyakua ushindi dhidi ya hali hizo. Usifadhaike maisha yajapo kukujaribu na kumbuka kuanguka si kushindwa. Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena. Pigana vita vizuri vya imani. Jitie nguvu katika vita na ukumbuke kuwa siku yako kuu haitakuja hadi ukabiliane na ushinde jaribu lako kuu.
Ombi la leo.
Baba, Neno lako Linasema kwamba nikizimia katika siku ya majaribu basi nguvu zangu ni kidogo. Nakuomba unifanyishe mazoezi, uninyooshe na unifanye kuwa sambamba kwa kunipa majaribu ninayoweza kukabiliana nayo maishani, si magumu sana, si rahisi sana, lakini inayotoshana na wakati na kiwango cha maisha yangu ili nikue. Nifunze njia zako.
Maandiko ya leo.
Mithali 24:16 Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba akaondoka tena; bali wasio haki hukwazwa na mabaya.
1 Timotheo 6:12 Piga mbio kadiri uwezavyo katika shindano la mbio za imani, ukajipatie tuzo la uzima wa milele, uliloitiwa wakati ulipokiri imani yako mbele ya mashahidi wengi.
1 Wakorintho 10:13 Majaribu mliyokwisha pata ni ya kawaida kwa binadamu. Mungu ni mwaminifu, naye hataruhusu mjaribiwe kupita nguvu zenu, ila pamoja na majaribu, yeye atawapeni pia nguvu ya kustahimili na njia ya kutoka humo salama.
2 Wakorintho 4:17 Taabu tunayopata ni kidogo, tena ya muda tu: lakini itatupatia utukufu upitao matazamio yote, utukufu ambao hauna mwisho.

Comments

Popular posts from this blog

SABABU 100 ZA UKWELI WA SUALA LA SABATO

JINSI YA KUINUA VIZAZI VINGI