Posts

Showing posts from May, 2016

Sababu Arobaini za Biblia Kuhusiana na Siku ya Kwanza ya Juma

1.  Kitu cha kwanza kabisa kilichowekwa kwenye kumbukumbu za Biblia ni kazi iliyofanywa siku ya Jumapili, siku ya kwanza ya juma.  Mwanzo 1:1-5.  Hii ilifanywa na Mwumbaji mwenyewe. Ikiwa Mungu aliumba dunia siku ya Jumapili, je itakuwa ni vibaya kwetu kufanya kazi siku ya Jumapili? 2 . Mungu anawaamuru watu kufanya kazi siku ya kwanza ya juma.  Kutoka 20:8-11.  Je, ni makoa kumtii Mungu? 3.  Hakuna hata mzee wa zamani aliyepata kuitunza. 4.  Hakuna hata manabii watakatifu waliopata kuitunza. 5.  Kwa amri iliyofafanuliwa ya Mungu, watu wake watakatifu walitumia siku ya kwanza ya juma kama siku ya kawaida ya kufanya kazi kwa miaka 4,000, angalao. 6.  Mungu mwenyewe huiita “siku ya” kufanya kazi.  Ezekieli 46:1. 7.  Mungu hakupumzika katika siku hii. 8.  Hakuibariki kamwe. 9.  Kristo hakupumzika katika siku hii. 10.  Yesu alikuwa seremala ( Marko 6:3 ) na akafanya shughuli hiyo mpaka alipokuwa na miak...

SABABU 100 ZA UKWELI WA SUALA LA SABATO

Kwa nini kutunza siku ya Sabato? Ni nini kusudi la Sabato? Je, ilifanywa lini, nani aliifanya, na kwa ajili ya nani? Siku ipi ni Sabato ya kweli? Wengi hutunza siku ya kwanza ya juma, au Jumapili. Ni mamlaka gani ya Biblia waliyo nayo kwa kufanya hivyo? Wengine hutunza siku ya saba, au Jumamosi. Ni Maandiko gani waliyo nayo kwa kufanya hivyo?       Hapa kuna ukweli kuhusiana na siku zote mbili, kama zilivyoelezwa wazi wazi katika neno la Mungu. Sababu Sitini za Biblia Kuhusiana na Siku ya Saba 1.  Baada ya kufanya kazi siku sita za kwanza za juma katika kuumba dunia hii, Mungu mkuu alipumzika siku ya saba.  Mwanzo 2:1-3. 2.  Hii iliweka muhuri [katika] siku hiyo kama siku ya Mungu kupumzika, au siku ya Sabato, kama siku ya Sabato [basi] humaanisha siku ya kupumzika. Kwa kufafanua: Wakati mtu anapozaliwa siku fulani, siku hiyo huwa siku yake ya  kuzaliwa . Kwa hiyo wakati Mungu alipopumzika siku ya saba, siku hiyo ilikuw...

UKWELI KUHUSU SABA

Changamoto ya 7: TUNATUNZA JUMAPILI KWA SABABU BAADA YA YESU KUFUFUKA WANAFUNZI WALIABUDU JUMAPILI a) Tukio la wanafunzi ghorofani siku Yesu alipofufuka(Yohana 20:19-21) Wale wanaoamini kuwa kuabudu siku ya jumapili ni kuiheshimu siku aliyofufuka Yesu mara nyingi wanazungumzia tukio la wanafunzi waliokuwa ghorofani siku Yesu anafufuka! Kwao mkusanyiko huo ulikuwa ni “kusherekea kwa njia ya ibada ufufuko wa Bwana wao”. Dai hili linashangaza kwani maandiko yanatueleza hivi: Marko 16:9-11,14: “Naye alipofufuka alfajiri siku ya kwanza ya juma, alimtokea kwanza Mariamu Magdalene, ambaye kwanza alimtoa pepo saba. Huyo akashika njia akawapasha habari wale waliokuwa pamoja naye, nao wakali wanaomboleza na kulia. Walakini hao waliposikia kama yu hai, naye amemwona, hawakusadiki…..Baada ya hayo akawatokea watu wawili miongoni mwao, ana sura nyingine,…. Na hao wakaenda wakawapasha habari wale wengine, wala hao hawakusadiki. Baadaye akaonekana na wale kumi na mmoja walipokuwa wakila, akawakemea...